Ka Obama Vile! Watu wangu wa Kata ya Lusu...

Sunday, August 8, 2010
Watu wangu wa Kata ya Lusu waliniita Obama...walishangilia kwa bashasha ya hali ya juu lilipotajwa jina langu Dr. Hamisi Kigwangalla a.k.a 'Shimba Ngosha'. Basi nami sikuwaangusha, hakika niliunguruma kama simba dume, nilitoa hotuba ya ukweli iliugusa kila moyo wa mwana Lusu aliyekuwepo pale. 

Nata ilikuwa balaa, mpaka nashindwa kusema neno lolote lile...walinipokeaje?

Isanzu, mh....

KURA ZA MAONI NZEGA!

Jamani, Uchaguzi si mchezo si lelemamaaa...

Hili ni baadhi tu ya mabango yaliyotumika kuuza sura, sera na jina la mbegu mpya, bora na ya kisasa inayoitwa "Kigwangalla"...pale Nzega kwa wanaCCM.

Tabasamu hili liliupamba mji wa Nzega...

Nikiliangalia napata fikra za kuleta mapinduzi ya kiuchumi kwa watu wangu wa Nzega...Mungu nipe uwezo.

Nimejifunza mengi sana ila moja ni la msingi na halitatoka kifuani mwangu mpaka kufa - wapende wapiga kura wako maana wao ndiyo mtaji na msingi mkuu wa kazi ya kisiasa!