Kigwangala - Mtu wa Watu!

Wednesday, December 22, 2010
Mgombea Ubunge wa Nzega kupitia Chama Cha Mapinduzi ni mtu mcheshi, mwenye bashasha na anakubalika kwa watu wa makundi yote. Hapa anaonekana amekaa akiongea na bibi kizee wa Kijiji cha Ijanija, Kata ya Ijanija, kabla ya hapo alikuwa akielekea kuhutubia mkutano wa kampeni ambapo alisimamisha gari yake mara moja na kushuka kwenda kumsalimia kikongwe huyu ambaye alifurahi sana kumuona Kigwangalla kwa macho yake!

Watoto Wengi Wamepewa Jina la 'Kigwangalla' Jimboni Nzega!

 
Wakati wa kampeni za uchaguzi mkuu mwaka 2010, jimboni Nzega ambako mgombea Ubunge wa CCM Dk. Hamisi Kigwangalla, ambaye alipewa Utemi wa Makaranga Ng'wana Ng'washi walizaliwa watoto wengi na kupewa jina la 'Kigwangalla' kwa mapenzi na mvuto wa mgombea huyu wa CCM, ambaye mwisho wa siku aliibuka mshindi wa uchaguzi huo! Mpaka leo hii takriban watoto 32 wamezaliwa kila pande ya Nzega na kupewa jina la Mbunge huyo...Huyu anayeonekana pichani ni mtoto Kigwangalla ambaye alizaliwa katika kijiji cha Ijanija, kilichopo kata ya Ijanija, Wilayani Nzega. Pembeni yake ni Bibi wa mtoto huyo akiwa amemshika kichwani kaka mkubwa wa 'Kigwangalla'.