Sherehe za Kuadhimisha Kuzaliwa kwa CCM (5 Februari 2010) Zilivyofana Nzega

Tuesday, March 2, 2010
Asubuhi saa kumi na mbili kamili viongozi wa chama na serikali; wanachama, wakereketwa na wapenzi wa Chama Cha Mapinduzi wilayani Nzega walijidamka na kukusanyika kwenye viwanja vya ofisi ya CCM wilayani hapo, kwa malengo ya kushiriki kwenye matembezi ya hiari yaliyolenga kudumisha umoja na mshikamano miongoni mwa wanachama. Matembezi hayo yalifana sana na yalifanywa kuwa rahisi kwa kutumbuizwa na nyimbo za kuhamasisha zilizoletwa na wahamasishaji mahiri.

Picha hapa chini inawaonesha:- Kutoka Kushoto: Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Tabora, Mzee Hassan Wakasuvi akiwa na Makada wa CCM Wilaya ya Nzega, Ndg. Babu Rajabu Ahmed (ambaye pia ni Katibu Tawi wa CCM, Tawi la Nzega Mjini Magharibi), Dk. Hamisi Kigwangalla na Ndg. Salum Juma (ambaye pia ni Katibu Tawi wa CCM, Tawi la Nzega Mjini Mashariki). Picha hii ilipigwa mara baada ya watembeaji hawa kurejea kwenye viwanja vinavyozunguka ofisi ya CCM wilaya ya Nzega, ambapo matembezi haya yalianzia.

No comments:

Post a Comment