Kuoa Uchagani kuna raha zake!
Friday, May 21, 2010
wikiendi iliyopita mke wangu Mama Sheila na Mimi tulitembelewa na wageni. Wageni hao, wakwe zangu na mashemeji walituletea supu (mbuzi wawili) ya mzazi (mama Sheila) kwa ajili ya kunywa na kuleta maziwa ya kutosha. Hii ni baada ya kufurahishwa na ujio wa Mtoto wetu wa pili tuliyempa jina la Hawwah Kigwangalla. Hawwah ni jina la mama mkwe wangu.
Dk. Hamisi Kigwangalla na Kilimo Kwanza Nzega: Kilimo cha Pamba Kinawezekana!
Friday, May 21, 2010

Mradi unaelekea katika ujenzi wa kiwanda cha kuchambua pamba (cotton ginnery) mjini Nzega, kilimo cha mkataba kwa mwaka wa kilimo wa 2010/2011 ambao ni mwaka wa pili wa mradi na pia kutanuka zaidi na kuunganisha wilaya jirani ya Uyui.
Hizi ni harakati za mashirika na watu binafsi kujitokeza kuunga mkono azimio la Mh. Rais Jakaya Mrisho Kikwete la Kilimo Kwanza kwa vitendo. Na tayari mafanikio yameshaonekana. Ushirikiano huu utawaletea manufaa makubwa wakulima na taifa kwa ujumla. Wengine wengi zaidi tujitokeze. TUKISHIRIKIANA TUTAJENGA UCHUMI IMARA!
Subscribe to:
Posts (Atom)