Dk. Hamisi Kigwangalla Kutangaza Rasmi Nia ya Kuwania Ubunge wa Jimbo la Nzega 2010

Tuesday, March 2, 2010
Mwanasiasa machachari na chipukizi, Dk. Hamisi A. Kigwangalla, ambaye ni mkazi na mzaliwa wa wilayani Nzega, Tabora anajipanga kutangaza rasmi nia yake ya kuwania ubunge wa jimbo la Nzega kupitia chama cha mapinduzi. 

Dk. Kigwangalla, ambaye anajiweka kama ni mtu mwenye kupenda maendeleo, anayeona mbali na mwenye nia ya dhati ya kuwaendeleza wanaNzega na watanzania wenzake walio maskini zaidi, alikuwa na haya ya kusema: "...mungu akinijaalia ninapanga kutangaza rasmi nia yangu ya kuwania ubunge wa jimbo la Nzega kupitia CCM kwenye uchaguzi ujao (yaani wa Mwaka 2010), hili linakuja sana baada ya kufuatwa na kuombwa na watu mbalimbali wa rika tofauti tofauti....nimejifikiria sana na ninadhani kama kila kitu kitaenda sawa naweza kufuata ushauri wa watu, kwa sasa hivi bado nashauriana na familia yangu, ndugu, jamaa na marafiki, wakiona nisonge mbele basi ninapanga kutangaza hadharani kupitia vyombo vya habari mnamo wiki ya kuanzia Machi 08, 2010."

Dk. Kigwangalla ni mwanaharakati, mkulima na mjasiriamali kijana aliyezaliwa wilayani Nzega miaka takriban 35 iliyopita na ni msomi wa digrii tatu ikiwemo ya kwanza ya udaktari wa tiba za binadamu (Doctor of Medicine), ya afya ya jamii (MPH) na ya utawala wa biashara (MBA). Kwa sasa anajishughulisha na kilimo na mambo ya harakati za kuleta maendeleo kwa kinamama, watoto na makundi mengine yaliyo katika hatari zaidi.

Tarehe 5-2-2010: Maadhimisho ya Kuzaliwa kwa CCM Nzega

Sherehe za kuadhimisha miaka 33 tangu Chama Cha Mapinduzi (CCM) kizaliwe zilivutia na kufana sana pale wilayani Nzega ambapo mgeni rasmi siku hiyo alikuwa Mwenyekiti wa CCM wa Mkoa wa Tabora Mh. Hassan Wakasuvi. 

Sherehe hizo zilianza alfajiri ya siku hiyo ya tarehe 5/2/2010 (ambayo ndiyo siku ya kuzaliwa kwa CCM, chama tawala Tanzania) kwa Viongozi mbalimbali wa kimkoa wakiongozwa na Mwenyekiti Wakasuvi, Katibu wa CCM Mkoa Ndg. Iddi Ali Ame, Katibu wa UVCCM Mkoa wa Tabora Ndg. Julius, na wajumbe wengine wa Kamati ya Siasa Mkoa kushiriki maandamano ya mshikamano yaliyoanzia kwenye viwanja vya ofisi ya CCM wilaya na kuishia Kitangiri na baadaye ofisini ambapo mgeni rasmi alitoa hotuba fupi iliyolenga katika kuhamasisha mshikamano miongoni mwa wanachama wa CCM Nzega. 

Pia Viongozi wa Kiwilaya, wanachama, wakereketwa na wapenzi wa CCM Nzega walikuwepo. 

Kabla ya kuwasilisha hotuba yake, Ndg. Mwenyekiti Wakasuvi na viongozi wengine wa CCM Mkoa na Wilaya walishiriki kupanda miti ili kuboresha mazingira ya ofisi ya CCM wilaya Nzega na kuweka alama ya ukumbusho.

Sherehe za Kuadhimisha Kuzaliwa kwa CCM (5 Februari 2010) Zilivyofana Nzega



Mh. Asha Kabeke (kwenye kiti) wa Kundi la 'Hiari Stars' akikata mauno na Mh. Diwani mwenzake.

Mwenyekiti Wakasuvi (Kulia) akiwa na Mh Diwani Basilio (Katikati) na Kada wa Chama

Sherehe za Kuadhimisha Kuzaliwa kwa CCM (5 Februari 2010) Zilivyofana Nzega

Asubuhi saa kumi na mbili kamili viongozi wa chama na serikali; wanachama, wakereketwa na wapenzi wa Chama Cha Mapinduzi wilayani Nzega walijidamka na kukusanyika kwenye viwanja vya ofisi ya CCM wilayani hapo, kwa malengo ya kushiriki kwenye matembezi ya hiari yaliyolenga kudumisha umoja na mshikamano miongoni mwa wanachama. Matembezi hayo yalifana sana na yalifanywa kuwa rahisi kwa kutumbuizwa na nyimbo za kuhamasisha zilizoletwa na wahamasishaji mahiri.

Picha hapa chini inawaonesha:- Kutoka Kushoto: Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Tabora, Mzee Hassan Wakasuvi akiwa na Makada wa CCM Wilaya ya Nzega, Ndg. Babu Rajabu Ahmed (ambaye pia ni Katibu Tawi wa CCM, Tawi la Nzega Mjini Magharibi), Dk. Hamisi Kigwangalla na Ndg. Salum Juma (ambaye pia ni Katibu Tawi wa CCM, Tawi la Nzega Mjini Mashariki). Picha hii ilipigwa mara baada ya watembeaji hawa kurejea kwenye viwanja vinavyozunguka ofisi ya CCM wilaya ya Nzega, ambapo matembezi haya yalianzia.