Tarehe 5-2-2010: Maadhimisho ya Kuzaliwa kwa CCM Nzega

Tuesday, March 2, 2010
Sherehe za kuadhimisha miaka 33 tangu Chama Cha Mapinduzi (CCM) kizaliwe zilivutia na kufana sana pale wilayani Nzega ambapo mgeni rasmi siku hiyo alikuwa Mwenyekiti wa CCM wa Mkoa wa Tabora Mh. Hassan Wakasuvi. 

Sherehe hizo zilianza alfajiri ya siku hiyo ya tarehe 5/2/2010 (ambayo ndiyo siku ya kuzaliwa kwa CCM, chama tawala Tanzania) kwa Viongozi mbalimbali wa kimkoa wakiongozwa na Mwenyekiti Wakasuvi, Katibu wa CCM Mkoa Ndg. Iddi Ali Ame, Katibu wa UVCCM Mkoa wa Tabora Ndg. Julius, na wajumbe wengine wa Kamati ya Siasa Mkoa kushiriki maandamano ya mshikamano yaliyoanzia kwenye viwanja vya ofisi ya CCM wilaya na kuishia Kitangiri na baadaye ofisini ambapo mgeni rasmi alitoa hotuba fupi iliyolenga katika kuhamasisha mshikamano miongoni mwa wanachama wa CCM Nzega. 

Pia Viongozi wa Kiwilaya, wanachama, wakereketwa na wapenzi wa CCM Nzega walikuwepo. 

Kabla ya kuwasilisha hotuba yake, Ndg. Mwenyekiti Wakasuvi na viongozi wengine wa CCM Mkoa na Wilaya walishiriki kupanda miti ili kuboresha mazingira ya ofisi ya CCM wilaya Nzega na kuweka alama ya ukumbusho.

No comments:

Post a Comment