Are we Realistically Trying to Solve the Electricity Problem in Our Country?

Tuesday, June 7, 2011
Mpaka leo hii, tuna mitambo ya jumla ya MW 336 inayowashwa kwa kutumia gesi asilia, yaani kuna ile inayomilikiwa na kuendeshwa na Songas (MW 191), ile ya serikali ya Ubungo (MW 100) na ile ya Tegeta (MW 45). Hii mitambo tu ukiongeza na ile ya makampuni kama matatu hivi yanayotumia gesi asilia kuendeshea mitambo yao, yameisha-exhaust supply ya gesi. Hata ile ya Dowans ikiwashwa leo, bado haitoweza kuwaka to full capacity (ya 112 MW), badala yake itazalisha MW 75 tu, kwa sababu ya poor supply ya gesi.

Leo hii kuna miradi ya Ubungo - MW 100, Kinyerezi MW 260 na Somanga Fungo MW 240, jumla yake ni MW 600. Je, serikali iko tayari kuwekeza kwenye bomba jipya litakalosaidia kutatua tatizo hili la upatikanaji wa gesi, ambalo ni very expensive?

Leo hii serikali inalalamikia gharama za uendeshaji wa mitambo ya IPTL, inayotumia Heavy Fuel Oil (HFO) kuwa ziko juu sana, sasa kwa nini tena inajenga power plant ya Mwanza (MW 60) kwa mitambo itakayotumia HFO ilhali wanaiona IPTL inavyosumbua kwa gharama?

Saa nyingine unashindwa kuelewa ni jinsi gani wasomi wetu wanafanya maamuzi mazito kama haya! Sijui wanakuwa wanatumia vigezo gani?

Hivi kwa nini serikali isianzishe mradi wa Umeme na wakajikita zaidi kwenye MW chache tu zilizo ndani ya uwezo wetu? Kama walivyofanya kwenye barabara kwa nini wasifanye hivyo pia kwenye umeme???

No comments:

Post a Comment